Islamic Calender

Powered by Blogger.

ELIMU YA HADITHI.


UCHAMBUZI YAKINIFU JUU YA ELIMU YA HADITHI.


Kabla ya kuanza kuzitaja hoja na dalili wanazozitegemea Ahli sunna
wal- Jamaa juu ya kuonekana Allah kwa macho huko akhera,
kwanza napenda kuzungumzia suala linalofungamana na elimu ya
istilahi ya upokezi wa riwaya za hadithi za bwana Mtume -swalla
llaahu alayhi wasallam- na suala hili litakuwa katika nukta
zifuatazo:

i) Kwanza, tufahamu kuwa mafundisho yote ya bwana Mtume -
swalla llaahu alayhi wasallam- ni wah’yi (ufunuo) utokao kwa
Allah, na Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- hazungumzi kwa
matashi wala matamanio ya nafsi yake.

ii) Pili, mafundisho yote ya Mtume wetu Muhammad -swalla llaahu
alayhi wasallam- yamehifadhiwa katika vitabu vya maulamaa wa Ahlu
Sunna wal-Jamaa kwa ufanisi mkubwa mno kiasi ambacho hakuna
jambo lolote linalohitajika kubainisha itikadi au hukumu ya mambo ya
dini ya kiislamu isipokuwa jambo hilo limedhibitiwa kwa ufanisi wa
hali ya juu.

iii) Tatu, katika kuhakikisha kuwa mafundisho hayo sahihi ya dini ya
kiislamu yanahifadhiwa na hayachanganyiki na upotofu wowote,
maulamaa wa Ahli Sunna wal Jamaa wameweka misingi madhubuti
juu ya usahihi wa mapokezi hayo ya riwaya za hadithi za bwana
Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- na ukweli wa wapokezi hao
kama tulivyofundishwa na Qur’an tukufu pale aliposema Allah:
ياأيها الذين آمنوا إن جاءآم فاسق بنبإ فتبينوا
“Enyi mlioamini ! akikujilieni mwovu (fasiki) na habari yoyote basi ichunguzeni”
al Hujraat (49) aya 6.
22
Kwa mujibu wa aya hii ni kwamba, si kila asemaye; amesema
Mtume -swalla llaahu alayhi wasallam- atakuwa msemaji huyo ni
mkweli, na atakayo yanukuu yatakuwa ni kweli maneno ya Mtume,
bali ni lazima uchunguzi wa kina ufanyike ili kujua usahihi wa habari
hiyo aliyoileta na udhaifu wake.
Kwa sababu hiyo, maulamaa wa hadithi baada ya kufanya utafiti wa
kina pamoja na kutumia uzoefu wao wa muda mrefu, wakaweka
misingi madhubuti inayowahusu wapokezi wa hadithi.
Pia wakaweka kanuni maalumu kwa ajili ya udhibiti wa njia sahihi
za kukubaliwa hadithi na kurudishwa.
Na pia yakatumika maneno ya kiistalahi ambayo yanaleta maana
maalumu na hayo yamejaa kwa wingi katika vitabu vyao.
Kwa mantiki hiyo, yeyote anayetaka kuzungumzia masuala
yanayofungamana na elimu ya hadithi; usahihi wake na udhaifu
wake, hana budi kuzijua kanuni hizo na maneno hayo ya kiistilahi.
Na kama hatafanya hivyo, basi lililobora kwake ni kunyamaza kuliko
kusema, kwa sababu hatima yake ni kupotosha watu kwa
kuzisahihisha hadithi zisizo sahihi au kuzidhoofisha hadithi zilizo sahihi
na yote mawili ni balaa, hasa ukizingatia kwamba maneno ya Mtume
Muhammad -swalla llaahu alayhi wasallam- ni sheria.
MASHAR’TI

YA USAHIHI WA HADITHI

العدالة ( 1 Uadilifu, ni lazima kila mpokezi wa hadithi za Mtume -
swalla llaahu alayhi wasallam- awe ni mtu mwenye akili
timamu,mwenye uwezo wa kupambanua mambo hata kama ni mtoto
mdogo, awe mkweli, mcha mungu na wala asiwe mwongo, zenye
kuvunja heshima.
23

تمام الضبط ( 2 Hifdhi nzuri wala asiwe mwenye kufanya maasia kwa
dhahiri wala asiwe na tabia mbaya
, mpokezi awe na uwezo wa kudhibiti maneno aliyo yapokea, bila
ya kubadilisha chochote katika maana yake,au kukosea sana,au
kubabaika kulikopetuka mipaka wakati wa kusimulia mapokezi hayo.

اتصال السند ( 3 Kuungana kwa sanadi (msururu wa wapokezi) kwa
kuwa kila mpokezi awe amepokea kutoka kwa aliye juu yake mpaka
mwisho wake (kwa huyo ambaye habari hiyo imenasibishwa kwake,
ima bwana -Mtume swalla llaahu alayhi wasallam-, au swahaba,
n.k.

عدم الشذوذ ( 4 Isiwe habari aliyoileta mpokezi huyo ni “SHAADHUN”
(ni yenye kupingana na habari ya mpokezi mwingine aliye madhubuti
au wengi zaidi kuliko yeye).

عدم العلة الخفية القادحة ( 5 Wala isiwe na ila (kasoro iliyojificha) kama
vile Idh’tiraabu (mgongano baina ya wapokezi n.k) au kuwa ni
habari Maq’luub (yenye kugeuzwa)
Katika masharti haya tuliyoyataja, yako ambayo likikosekana moja tu
basi hadithi haitakubaliwa,kama vile:
1-Kuwa mpokezi si muadilifu,kwa kuwa ni mwongo au asherati n.k.
2-Kupatikana kasoro kama vile mgongano katika sanadi (njia) au
mgongano wa maneno katika habari hiyo, kisha ikawa imeshindikana
kuziunganisha au kuipa nguvu njia moja juu ya nyingine.
Tanbihi:
Habari inaweza kuwa na njia nyingi, na katika njia hizo wakawepo
wapokezi wasio madhubuti kwa kuwa wanakosea kiasi, au silsila
(mtiririko) wa wapokezi haukuungana, kutokana na wingi wa njia
hizo habari hiyo itapata uzito na kuhesabiwa kuwa ni sahihi, na kwa
lugha ya kitaalamu huwa wanaiita “HASANUN-LIGHAIRIHI”.
24
Amesema Imamu An-Nawawiy:
"بل ما آان ضعفه لضعف حفظ راويه الصدوق الأمين من وجه آخر وصار حسناً وآذا إذا آان ضعفها
لإرسال زال بمجيئه من وجه آخر...".
“Bali ile hadithi ambayo imekuwa ni dhaifu kwa sababu ya udhaifu
wa mpokezi wake ambaye ni mkweli mwaminifu utaondoka (udhaifu
huo) kwa kuja kwake kupitia njia nyingine na itakuwa ni HASAN
(sahihi)
Na vile vile ukiwa udhaifu wake ni kwa sababu ya Ir’saal
(atakaposema Taabi’I amesema Mtume -swalla llaahu alayhi
wasallam-) pia udhaifu huo utaondoka kwa kuja (kupokewa) kwa
njia nyingine…”.
Hivyo basi, inawezekana ukaifuatilia hadithi kisha ukazikuta takriban
njia zake zote zina udhaifu, hapo hutakiwi kuwa na pupa na kuanza
kuihukumu hadithi yote kuwa ni dhaifu, bali unatakiwa kuihukumu
sanad husika tu, na useme kwamba sanad ya hadithi hii ni dhaifu.
Kwa sababu udhaifu wa sanad moja tu, si ushahidi wa udhaifu wa
hadithi yote yenye njia nyingi.
Na kama ukitaka kuihukumu hadithi yote kwa njia zake zote
unatakiwa ufanye kazi ya kuzikusanya sanad (njia) zote kisha ndiyo
uichambue sanad moja baada ya nyingine kwa kufuata kanuni na
taratibu za elimu ya hadithi (mustalahul-hadithi).
Na kama itakubainikia kuwa njia zote zina udhaifu, basi pia
unatakiwa kuangalia sababu za udhaifu wake.
Je udhaifu wake ni mwepesi au mzito?
Kama ni mwepesi basi hadithi hiyo kwa kuzijumuisha njia zote hizo
itakuwa ni “Hasanun-Lighayrihi” (sahihi) na itafaa kuifanya kuwa ni
hoja ya kisheria, na wala haitohesabiwa kuwa ni dhaifu.
Hili ni jambo muhimu sana katika elimu ya hadithi kulifahamu na
kulizingatia, lakini ndugu Juma kwa makusudi hakuuzingatia utaratibu
huu kwenye kitabu chake “Hoja zenye Nguvu” kwa sababu
anazozijua mwenyewe, kwani yeye ndiye aliyesema hivi:
25
“kitaalamu ikiwa hadithi imepokewa na wapokezi wengine kabisa,
lakini hadithi ni ile ile, basi huambiwa kuwa hadithi hiyo ina
shahidi.”
Mwisho wa kunukuu.
Tazama “Hoja zenye Nguvu” ukurasa 70.
Lakini huko mbele -Inshaallah- utazigumdua sababu zilizomfanya
ndugu Juma aupuuze utaratibu huu.
Source: hoja zenye nguvu katika kuthibitisha kuonekana allah(S.W) kwa macho huko akhera_Ukurasa 20-25)

Comments :

0 comments to “ELIMU YA HADITHI.”

Post a Comment

 

Website Hit