Islamic Calender

Powered by Blogger.
Showing posts with label Makala. Show all posts
Showing posts with label Makala. Show all posts

MU'TA NDOA YA HARAMU


Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu,bwana wa viumbe wote,na reh'ma na amani zimfiukie Mtume wetu Muhammad bin Abdillahi mbora wa viumbe wote,na ziwafikie jamaa zake na wake zake,na maswahaba zake wote kwa ujumla.
Ama baada ya utangulizi;
Jambo la familiya ni katika mambo muhimu sana,katika jamii ya kiislamu,na ndiyo maana Qur'ani imelizungumzia jambo hili katika pande zote,na Sunna ikasherehesha,na kufafanua na kuelezea kwa undani zaidi makusudio hayo ya Qur'ani.
na katika mambo muhimu yaliyo fafanuliwa kwa uwazi katika  Qur'ani na Sunna ni nidhamu kamili ya familia,
Qur'an na Sunna zimebainisha nidhamu hiyo kwa mpango ufuatao;
1- Qur'an na Sunna zimebainisha malengo matukufu ya ndoa.
2- mahimizo juu ya ndoa.
3- sifa za mume/mke mwema.
4- taratibu za kufanya iwapo utakosekana uwezo wa kuoa.
5- taratibu zote za kutimiza suala la ndoa.
6- haki za mke na mume,na wajibu wa kila mmoja.
7- namna ya kuyalinda mahusiano ya ndoa kati ya mke na mume.
8-mtazamo juu ya familia kabla ya uislamu na baada ya uislamu.
9- na suala la kuoa zaidi ya mke mmoja.
hukumu hizi zote zimefafanuliwa vizuri katika Qur'ani na Sunna kwa ufafanuzi wa wazi kabisa,tena ulio kamilika.
hivyo basi hakuna suala lolote katika hukumu za ndoa linalo hitajika halafu likawa halina ufafanuzi wa kisheria,
kwa mantiki hiyo basi,itakuwa haingii akilini kabisa,kuwa eti Qur'an na Sunna zimeruhusu Mut'a,halafu hakuna ufafanuzi wowote ule juu ya suala hili,kuanzia suala la kuwepo walii katika kufungisha ndoa,mashahidi hadi kufikia suala la kurithiana au kutokuwepo,
tena ndoa yenyewe iwe imehalalishwa kwa ishara ya mbali kiasi ambacho mpaka hao maulamaa wa tafsiri wenyewe hawaja wafikiana juu ya maana ya Aya hiyo,kama tutakavyo elezea hili mahala pake.
na wala hakuna tafsiri yoyote kutoka kwa Mtume (s.a.w.) inayoelezea kwamba Aya hiyo maana yake ni ndoa ya Mut'a, wala hakuna hadithi yoyote sahihi inayo bainisha hukumu,na taratibu za ndoa hiyo,si kwa ujumla wala kwa taf'sili !!
matokeo yake ndiyo wakajitokeza baadhi ya watu kwasababu ya tamaa,na matamanio ya nafsi zao wakaamua kutunga sheria zao kutoka akilini mwao.
na hilio ni baada ya kukosa katika kitabu cha Allah na Sunna za Mtume wake (s.a.w.) upambanuzi yakinifu juu ya suala zima juu ya ndoa ya Mut'a !
ndiyo ukawa unawasikia wale wenye kuihalalisha ndoa hiyo haramu (kama Omar Mayunga na Abdillahi Nassir)
wakisema kuwa;
-Ndoa ya Mut'a haihitaji kusimamiwa na walii !
swali; je,ni kwa aya gani au kwa hadithi ipi ya Mtume Muhammad (s.a.w.) iliyojuzisha hilo?
au ni maoni binafsi?
je,hao walio jiwekea sheria hiyo wana nafasi gani katika dini hii ya kutunga sheria wazitakazo wao?
Allah anasema;
فانكحوهن بإذن أهلهن ....
(waoeni hao wanawake kwa idhini ya mawalii zao....) al maida aya 25.
na Bwana Mtume (s.a.w.) anasema;
Mwanamke yoyote atakaye jiozesha mwenyewe,bila idhini ya walii wake,basi mwanamke huyo ni mzinifu).
na katika riwaya nyingine inasema;(basi ndoa hiyo ni batili..).
huwenda watetezi wa ndoa hii ya haramu wakasema;
hiyo ni hukumu ya ndoa za kudumu,lakini Mut'a ina hukumu tofauti na ndoa hizo...
swali hukumu kaziweka nani? kwa ushahidi gani?
na ama kauli ya mwanawachuoni yoyote iliyo kinyume na kauli ya Allah na Mtume wake (s.a.w.) haitokubalika,na hukumu hiyo itakuwa ni batili kwa kuhalifu kauli ya Allah na Mtume (s.a.w.).
pia mtawasikia wakisema;
Ndoa ya Mut'a haihitaji kuwepo mashahidi !!
na hali ya kuwa Mtume (s.a.w.) anasema;
hakuna ndoa -itakayo sihi- bila ya walii na mashahidi wawili.
ameipokea hadithi hii Imam Ahmad katika musnadi yake,tazama Ir'waul ghalil juz 6/258-261.
pia mtawasikia wakisema;
Hakuna kurithiana -baina ya mke na mume katika ndoa ya Mut'a- anapokufa mmoja wao!
tazama kitabu Mut'a ndoa sahihi cha Mayunga uk 2.
na bila shaka hukumu ya Allah na Mtume wake ni tofauti na hukumu hii ya kina Mayunga,amesema Allah (s.w.t.);
(N a nyinyi mtapata nusu ya walichoacha wake zenu....)
na amesema kuhusu wanawake;
(nao -wake zenu- watapata robo ya mlicho kiacha...).
na hukumu hii ndiyo asili katika ndoa,kuwa wanandoa wanarithiana,na ila kitakapo patikana kizuwizi chochote cha kisheria kitakacho zuia kurithiana,kama vile;
mke kumuua mumewe au mume kumuua mke,muuaji hatomrithi mwenziwe.
au mmoja wao kuwa ni mtumwa,aliye mtumwa hatorithi.
au tofauti za dini,
na ama Mut'a ni kinyume kabisa na ubainifu huu wa Mtume (s.a.w.) hakuna katika ndoa hiyo ya haramu kurithiana kabisa, ni mamoja kuna sababu au hakuna ! na hukumu hiyo si Allah wala Mtume (s.a.w.) bali ni hukumu ya kina Mayunga na kundi lake,ndiyo pale wanapo hojiwa; ni ndoa gani basi hiyo isiyo na walii,mashahidi,wala kurithiana? badala ya kutoa ushahidi wa Qur'ani au Sunna sahihi za Mtume (s.a.w.) utawaona wanakwenda mbio huku wakitweta huku wakisema;
mbona Abu Hanifa kasema kwamba ndoa bila ya walii yafaa?!
Ibin Mundhir kasema haikuthibiti habari yoyote (sahihi)katika kushuhudia ndoa... !!
لاmwanamke wa ah'lulkitabi aliyeolewa na mwislamu,hawezi kumrithi mumewe...!!
hayo ndiyo majibu yao,badala ya kutoa hoja na dalili,wao hutumia ujanja ujanja katika dini.
sisi tunasema kwamba;lau kama Mut'a ni ndoa halali basi sheria ingebainisha hukumu zake,a-z,na wala isengehitajia ujanja ujanja wakina Mayunga na kaumu yake.
kama Abu Hanifa amesema kwamba ndoa bila ya walii inafaa,swali je Mtume (s.a.w.) anasemaje -ukiwa unamuamini-?



hoja zao za kuhalalisha ndoa hii haramu(Mut'a)


Hoja kubwa inayotolewa na wale wenye kuhalalisha ndoa hii ya haramu (Shia Ith'naasharia) ni aya ya 24 ya surat al nisaa isemayo;
فما استمتعتم به منهنّ فآتوهنّ أجورهنّ فريضة...) (
(Na ambao mmestarehe nao katika wao,basi wapeni mahari yao yaliyo lazimu...)

kisha husema kwamba wameafikiana wanawachuoni wote kwamba aya hii imeshuka kuhalalisha Mut'a,kisha wanakutajia mirundo ya vitabu vya tafsiri kama kawaida yao ili kuwababaisha wasio jua.
jawabu yetu ni kama ifuatavyo;
a) Aya hii haikuteremka kwa ajili ya kuhalalisha ndoa ya Mut'a,bali aya hii imekuja kuelezea hukumu ya ndoa ya kudumu kwamba iwapo mtawaoa wanawake kisha mkastarehe nao kwa kuwaingilia basi wapeni mahari yao kamili,kwasababu kiislamu ni kwamba mtu akimuoa mwanamke kisha ikatokea kwamba hakuwahi kumuingilia,basi anatakikana mwanamke huyo apewe nusu ya mahari na si mahari kamili,na kama mume atawahi kumuingilia mkewe basi atalazimika kutoa mahari kamili kama inavyoelezea ya hii.
b)kudai kwamba wanawachuoni wameafikiana juu ya tafsiri hiyo,huo ni miongoni mwa urongo wa kishia,na hakuna mwanawachuoni yoyote aliyeelezea maafikiano hayo,si mwanawachuoni wa kishia wala wa Ah'lusunn,bali mambo ni kinyume cha hivyo,bali wanawachuoni wa Ah'lu Sunna wameafikiana kwamba aya hii haizungumzii ndoa ya Mut'a kwa hoja na dalili,tutazija katika sehemu yake.
amesema Imamu Ibin Jarir Twabari baada ya kutaja kauli mbili za wanawachuoni juu ya tafsiri ya aya hii;
(Na tafsiri iliyo bora katika tafsiri mbili hizi,na iliyo sawasawa,ni tafsiri ya mwenye kutafsiri hivi;
Na wale ambao mmewaona katika hao -wanawake- na mkawaingilia,basi wapeni mahari zao.
kwasababu ya kusimama hoja ya  kuharamisha Mwenyezi Mungu kustarehe na wanawake bila ya kutumia njia zilizo sahihi za ndoa,au bila umiliki sahihi,-ameliharamisha hilo- kupitia ulimi wa Mtume wake (s.a.w.)
tazama tafsir Twabari juz 5 uk 19.

HISTORIA YA MAWLID

HISTORIA YA MAWLID
Yeyote mwenye kutazama maisha ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na historia ya Maswahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum), Taabi‘iyna na waliowafuata kwa wema mpaka kufikia zaidi ya mwaka wa 350 Hijri hatumuoni hata mwanachuoni mmoja wala mahakimu (viongozi) na wala watu wa kawaida waliokuwa wakifanya Mawlid au wakaamrisha au wakahimiza au wakazungumza juu yake. Amesema al-Haafidh as-Sakhawiy: “Shughuli za kufanya Mawlid matukufu hayakupokelewa na watangu wema (Salafus Swaalih) wa karne tatu bora za mwanzo. Kwa hakika jambo hili lilizuliwa baada yake” (Imenukuliwa kutoka kwa Subulul Hudaa war Rashaad cha As-Salihiy, Mj. 1, uk. 439).
Suala la sisi kujiuliza ni kuwa;
Je, haya Mawlid yalianza lini?
Jawabu ya suala hili kwa mwanachuoni wa Ki-Sunnah, Al-Imaam al-Maqriiziyni:
“Katika kipindi cha uongozi wa Faatwimiyyuun (hawa walikuwa ni Rawaafidh (Mashia) katika kipote cha Ismailiyyah [Makoja] katika nchi ya Misri) walikuwa wanachukuwa hii ni misimu ya sherehe ambapo walikuwa wakiwakunjulia hali za raia zao na kuwakithirishia neema. Na walikuwa hawa watawala wa Faatwimiyyuun katika mwaka mzima wana misimu ya sherehe na Idi zao nazo ni kama zifuatazo: Msimu wa kichwa cha mwaka, Msimu wa mwanzo wa mwaka, Sherehe za ‘Aashuraa, na Mawlid ya Nabii (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na Mawlid ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (Radhiya Allaahu ‘anhu), na Mawlid ya Hasan na Husayn (Radhiya Allaahu ‘anhuma), na Mawlid ya Faatwimah az-Zahraa (Radhiya Allaahu ‘anha), na Mawlid ya kiongozi wao aliye hai kwa wakati ule, usiku wa kwanza wa Rajab, na usiku wa kati ya Rajab, na Mawlid ya usiku wa Ramadhaan na mwisho wa Ramadhaan na Msimu wa 'Iydul Fitwr na Msimu wa 'Iydul Adh-ha na Idi ya Ghaadir, Msimu wa ufunguzi wa Ghuba na Siku ya Nairuuz na Siku ya Ghatas na Siku ya Mazazi, na Siku ya Vipandio, Kis-wa (nguo) ya Msimu wa Kusi na Kaskazi, Alhamisi ya Adasi na Siku ya Ubatizo” (Al-Khutwat, Mj. 1, uk. 490 na baada yake). na amesema tena katika kitabu chengine: “Na katika mwezi wa Rabi’ul Awwal walijilazimisha watu kuwasha kandili usiku katika njia zote na vichochoro vyake huko Misri”.
Na amesema tena al-Maqriiziy katika maudhui nyengine: “Shughuli za Mawlid ya Mtume mtukufu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) zilikuwa zikifanyika rasmi kama desturi yake katika mwezi wa Rabi’ul Awwal”. Kila mmoja anatakiwa azingatie jinsi gani Mawlid yalivyoanzishwa pamoja na uzushi mkubwa mfano: Uzushi wa kukataa na kuchupa mipaka juu ya familia ya Mtume kwa kusimamisha mawlid ya ‘Aliy, Faatwimah, Hasan na Husayn.
Uzushi wa kusherehekea Idi ya Nayruuz, na Idi ya Ghatas na kuzaliwa kwa Masihi nazo ni Idi za Wakristo. Amesema Ibn Turkumani kuhusu hizi Idi za Wakristo: “Na miongoni mwa uzushi inayoleta hizaya ni wanaofanya Waislamu katika siku ya Nayruuz ya Kikristo na misimu yao mengine na siku kuu (Idi) kwa kupeana chakula kwa wingi. Na sadaka ya chakula isiyokubalika itarudi kwa mwenye kutoa kwa haraka au baadae. Na kwa uchache wa tawfiki na kufaulu ni yale wanayofanya Waislamu waovu kwa inayotambuliwa kama siku ya mazazi (yaani kuzaliwa kwa Yesu)” (Al-Lam‘i Fil Hawaadith wal Bid’ah, Mj. 1, uk. 293 – 316). Na imenukuliwa kutoka kwa wanavyuoni wa Hanafiyyah kwamba yeyote ambaye atafanya mambo yaliyotangulia atakuwa kafiri mfano wao (hao Wakristo). Na wakataja idadi za Idi kadhaa za Wakristo ambao Waislamu walio wajinga wanashiriki, na jinsi zilivyo uharamu wake katika Kitabu na Sunnah na yale misingi ya kisheria yaliyo kamili.
Watu wa kwanza kuzua kile kinachoitwa Mawlid ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni Bani ‘Ubayd ambao walikuwa wakijulikana kama Faatwimiyyuun. Haya yametajwa na wanazuoni wengi mfano Mufti wa Misri wa zamani, Shaykh Muhammad Bakhiit al-Mutii‘y katika kitabu chake Ahsanul Kalaam Fi maa Yata‘alaq Bis Sunnah wal Bid‘ah Minal Ahkaam; Shaykh ‘Ali Mahfuudh katika kitabu chake Al-Ibda‘ Fii Madh-har al-Ibtidaa‘; Shaykh Isma‘iyl al-Answaariy katika kitabu chake Al-Qawlul Fasl Fiy Hukmil Ihtifaal Bi Mawlid Khayrir Rasuul.
“Wa mwanzo walioyazua Mawlid huko Cairo ni watawala wa Kifaatwimiyyah (Mashia) katika karne ya nne. Walizua Mawlid aina sita: Mawlid ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Mawlid ya Imam ‘Aliy (Radhiya Allaahu ‘anhu), Mawlid ya Bibi Faatwimah (Radhiya Allaahu ‘anha), Mawlid ya Hasan (Radhiya Allaahu ‘anhu), Mawlid ya Husayn (Radhiya Allaahu ‘anhu) na Mawlid ya Khalifa aliyekuwepo” (‘Ali Mahfuudh katika kitabu chake al-Ibda‘ Fii Madh-har al-Ibtidaa‘, uk. 251).
Je, wanazuoni wamesema nini kuhusu hii Dola ya Faatwimiyyuun ‘Ubaydiyyah ambayo imeanzisha jambo hili (Mawlid ya Mtume)? Amesema Imaam Shaamah, mwana-historia na Muhaddith (aliyeboboea katika mas-ala ya Hadithi za Mtume [Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam]), mwandishi wa kitabu ar-Rawdhatayn Fiy Akhbaar Dawlatayn, uk. 200 – 202 kuhusu Faatwimiyyuun ‘Ubaydiyyah: “Wao walijidhihirisha kwa watu kuwa wao ni masharifu (watukufu) kutoka kwa Faatwimah hivyo wakamiliki na kutawala ardhi na kuwatendesha nguvu waja. Na wametaja kipote cha wanazuoni wakubwa kuwa wao hawakustahiki hilo na nasaba yao si sahihi bali walikuwa wanajulikana zaidi kwa banu ‘Ubayd. Na baba wa ‘Ubayd alikuwa ni katika kizazi cha wakanaji Mungu na Mmajusi na inasemekana kuwa babake alikuwa Myahudi mfua vyuma kutoka Shaam. Jina la huyu ‘Ubayd lilikuwa ni Sa‘iyd, lakini alipofika Morocco alijiita ‘Ubaydullah na akajidai kuwa yeye ni katika ukoo wa ‘Alawi Faatwimiy na madai yake ya nasaba hiyo siyo sahihi. Yeye hakutajwa na yeyote miongoni mwa wajuzi wa nasaba za ‘Alawi, kipote kikubwa cha wanavyuoni wametaja kinyume cha hayo. Alijinasibisha na Bani Mahdiyyah wa Morocco, naye alikuwa Zindiyq muovu, adui wa Uislamu na alijidhihirisha Ushia wake. Alikuwa na hima ya kuiondoa mila ya Kiislamu pamoja na kuwaua mafaqihi wengi pamoja na wanavyuoni wa Hadiyth. Kusudio lake kubwa lilikuwa kuwaondosha kabisa ili dunia ibaki na wanyama pekee na hivyo kumakinika katika kuleta uharibifu katika itikadi zao na kuwapoteza lakini Allaah Anaitimiza nuru Yake japokuwa watachukia makafiri”. 
Kizazi chake kiliinukia katika hilo huku wakijitokeza wakati kukiwa na fursa na isipokuwa hivyo walikuwa wakijificha na kufanya vituko vyao kwa siri. Walinganizi wake walitumwa katika nchi yote huku wakiwapoteza wale wanaoweza miongoni mwa waja. Balaa hii ilibakia kwa Uislamu kuanzia mwanzo wa Dola yao mpaka mwisho wake yaani Dhul-Hijjah 299 hadi 567 Hijri.
Katika siku zao za utawala hawa Rawaafidh (Mashia) waliongezeka sana na hivyo wakawa wanahukumu watu kwa kuwawekea vikwazo na wakaweza kuharibu itikadi za mapote ya watu waliokuwa wakiishi katika majabali na mapango ya Shaam kama Nusayriyyah, Druze na Hashashiyyun (Assassins), wote wakiwa aina moja na wao wenyewe. Waliweza kuwatumia kwa sababu ya udhaifu wa akili zao na ujinga wao, hivyo kuwapatia fursa Wazungu (Crusaders â€“ watu wa msalaba) kuziteka ardhi za Shaam na Bara Arabu mpaka Allaah Alipowapatia Waislamu ushindi chini ya uongozi wa Swalaah ud Diyn Hasan al-Ayyubi ambaye aliweza kuzirudisha nchi hizo kwa Waislamu.
Makhalifa 14 walipita, ambao walikuwa wanajiita masharifu na nasaba yao ni kutokana na Majusi au Mayahudi mpaka likawa maarufu baina ya watu wa kawaida hivyo kuiita dola hiyo, Dola ya Faatwimah na Dola ya ‘Alawi na ilihali uhakika ni Dola ya Kimajusi au ya Kiyahudi wakanaji Mungu.
Na miongoni mwa uovu wao ni kuwa walikuwa wakiwaamrisha makhatibu kwa hilo (yaani wao ni Alawiyyah Faatwimiyyuun) na hayo yalikuwa yakisemwa juu ya minbar na wakiandika katika kuta za Misikiti na sehemu nyinginezo. Na alihutubu yeye mwenyewe mtumishi wao kwa jina Jawhar, aliyeteka nchi ya Misri na kujenga mji wa Cairo. Alisema ndani yake: “Ewe Mola mswalie mja wako na rafiki yako tunda la Unabii na dhuria wako mwenye kuongoza muongofu anayepelekesha mambo. Naye ni Abi Tamiym Imam Mu‘iz-ud-Diinil Llah, Amiri wa Waumini kama ulivyowaswalia baba zake walio tohara na waliomtangulia kwa kuchaguliwa, maimamu waongofu”. Amesema uongo adui wa Allaah, hakuna kheri kwake wala kwa watangu wake wote wala kwa dhuria wake waliobakia na kizazi cha Unabii tohara miongoni mwao.
Na yule mwenye lakabu ya Mahdi, laana ya Allaah iwe juu yake aliwachukuwa wajinga na kuwasalitisha kwao wale wenye fadhila.. Alikuwa akiwatuma kwenda kuwachinja mafakihi na wanavyuoni katika firasha zao. Na akawasaliti Waislamu kwa Warumi na alikuwa na ujeuri mwingi na kuchezea mali na kuwaua watu. Alikuwa na kipote cha walinganizi (ma-Du‘aat) wake waliokuwa wakifanya kazi ya kuwapoteza watu kwa uwezo wao wote.. Wao walikuwa wakiwaambia baadhi ya watu: “Huyo ni Mahdi mtoto wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na dalili (huja) ya Allaah kwa viumbe vyake”. Na kwa wengine: “Huyu ni Mtume wa Allaah na dalili ya Allaah”. Na kwa wengine: “Yeye ni Allaah, Muumbaji, Mwenye kuruzuku”. Hapana Mola muabudiwa wa haki ila Allaah tu, Naye Hana mshirika, Ametukuka na Hana upungufu wala kasoro aina yoyote kwa yale wanayoyasema madhalimu kwa kiburi kikuu. Alipoangamia alichukua hatamu za uongozi mtoto wake anayeitwa, Qa’im, naye alizidisha shari yake juu ya uovu wa babake maradufu. Akatoka na kuwatusi Manabii na alikuwa akinadi masokoni na sehemu nyenginezo: “Mlaanini ‘Aishah na mumewe. Mlaanini pango na vinavyounganishwa”.
Ewe Allaah! Mswalie Nabii Wako na Maswahaba zake na wakeze walio twahara na uwalaani hawa makafiri walioasi na kuvuka mipaka katika ukanaji wa Mwenyezi Mungu na Uwarehemu waliopambana nao na ikawa ndio sababu ya kuing’oa mizizi na utawala wao. Waislamu katika zama za utawala wao walipata dhiki na shida kubwa kwa ukatili, kiburi na ujeuri wao uliochupa mipaka.
Na juu ya Mawlid ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kama tulivyoona asli yake na mwanzilishi wake ni kutokamana na Baatwiniyyuun (Faatwimiyyuun) waliokuwa na asli ya Kimajusi Kiyahudi waliohuisha mwito wa watu wa msalaba. Na hapa tunawaambia ya kwamba: Je, inajuzu na kusihi kuifanya chimbuko letu katika 'Ibaadah ni kutoka kwa watu hawa? Nasi tunarudia mara nyingine tena kuwa zile karne zilizo bora na kufadhilishwa ambazo waliishi watangu wetu wema hakukuwa na athari wala kufanywa mfano wa hizi 'Ibaadah. Hawakufanya wao wala wale waliokuwa na uadui nao na hata wale wajinga katika watu wa zama hizo na watu wa kawaida. Basi nasi hatujishughulishi katika yale waliyoyafanya na kujishughulisha nayo wao.
Naye Shaykh 'Abdulla Saleh Farsy (Allaah Amrehemu) katika kuelezea yalivyoanza Mawlid anasema:
"Walioanza Mawlid ni watu wenye Madhehebu za Kishia, hawa Shia Ismailiya walizitawala nchi za Kisuni tangu mwaka 297 A.H. (909) mpaka 567 A.H. (1171) (muda wa miaka 270).
Walipotoka katika nchi hizo waliacha hiyo ada yao ya kumsomea Mawlid Mtume na Maimamu zao. Basi Suni wakaendeleza Mawlid ya Mtume, wakayawacha yote mengine.
Mawlid ya Mwanzo Rasmi Kusomwa na Suni:
Mawlid ya mwanzo Rasmi yalisomwa na Suni ni Mawlid aliyokuwa akiyasoma Mfalme Mudhaffar Din- Mfalme wa kaskazi ya Iraq ambaye alikuwa shemeji wa mfalme mkubwa wa Kiislamu, Mfalme Salahud Din (Saladin - maarufu). Mawlid makubwa kabisa hayo. Yalikuwa yanahudhuriwa na watu wa pande zote zilizokuwa karibu na hapo, kwa shangwe kubwa kabisa lisilokuwa na mfano.
Mfalme huyo alizaliwa mwaka 549 A.H. (1154 wa kizungu); na akatawala hapo mwaka 586 A.H. (1190) na akafa 630 A.H. (1233) - miaka mia saba na khamsini na sita (756) kwa tarikhi ya kiislamu, na miaka mia saba na thalathini na tatu kwa tarikhi ya Kizungu. Basi ada ya kusoma Mawlid haikuanza miaka mingi sana. (Tafsiri ya Mawlid BARZANJI - KADHI SHEIKH ABDULLA SALEH FARSY, ZANZIBAR, Uk.(iv) )

Sababu za Kutosherehekee Maulidi-Sehemu ya Kwanza


 sehemu ya kwanza
Sababu 21 Za Kumfanya Muislam Asisherehekee Maulid
 Zifuatazo ni sababu na hoja ambazo Muislam mwenye kupenda kufuata haki na mwenye kutaka apate uongofu ili abakie katika njia iliyonyooka na ajiepushe na mambo ya baatil. Hoja ni za wazi kutoka katika Qur-aan na Sunnah. Hoja za kupinga jambo hili ziko nyingi sana, lakini tulizozikusanya tunatumai kuwa zitamtosheleza Muislamu aikinaishe nafsi yake kuwa Maulidi ni jambo la uzushi katika dini kwa hiyo ni bora kutenda amali zile tulizopata mafundisho yake kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم, Maswahaba wake na Salafus Swaalih (Watangu wema) .
SABABU YA KWANZA: Kumpenda Mola Mtukufu Aliyetuumba:
Kwanza kabisa ni kwa sababu  ya kumpenda Mola Mtukufu Aliyetuumba Ambaye Anataka kuhakikisha kuwa mapenzi yetu Kwake ni kumfuata Mtume صلى الله عليه وآله وسلم. Naye tokea kuzaliwa kwake hadi kufa kwake hakufanyiwa wala hakusherehekea siku yake ya kuzaliwa. 
 Anasema Allaah سبحانه وتعالى :
 ((قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللّهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللّهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَاللّهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ)) 
 ((Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allaah basi nifuateni mimi, Allaah Atakupendeni na Atakufutieni madhambi yenu. Na Allaah ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu)) [Al-'Imraan: 31] 
 SABABU YA PILI: Kufuata amri yake Mtume صلى الله عليه وآله وسلم    ya kushikamana na Sunnah Zake na Sunnah za Makhalifa wake:
 (( أُوصِيكُمْ بِتَقْوى اللَّه، وَالسَّمْعِ وَالطَّاعَةِ وإِنْ تَأَمَّر عَلَيْكُمْ عَبْدٌ حبشيٌ ، وَأَنَّهُ مَنْ يَعِشْ مِنْكُمْ فَسَيرى اخْتِلافاً كثِيرا . فَعَلَيْكُمْ بسُنَّتي وَسُنَّةِ الْخُلُفَاءِ الرَّاشِدِينَ الْمَهْدِيِّينَ ، عضُّوا عَلَيْهَا بالنَّواجِذِ ، وإِيَّاكُمْ ومُحْدثَاتِ الأُمُورِ فَإِنَّ كُلَّ بِدْعَةٍ ضلالَةٌ ))  رواه أبو داود ، والترمذِي وقال حديث حسن صحيح
((Nakuusieni kumcha Allah, usikivu na twaa hata ikiwa kiongozi wenu (Au atakayekuamrishen) ni Mtumwa  wa Habash. Mtakaoishi miongoni mwenu mtaona ikhtilafu nyingi. Kwa hiyo shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa waliongoka baada yangu.  Ziumeni kwa magego (zikamateni kwa nguvu wala msiziache). Na tahadharini na mambo ya uzushi kwani kila bid'ah ni upotofu)) [Abu Daawuud, At-Trimidhiy kasema Hadiyth Hasan Swahiyh]   
Kwa hiyo inamtosheleza Muislamu hoja hii pekee ya kuwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم wala Maswahaba zake hawakusherehekea Maulidi, kumfanya naye asisherehekee.
Na hiyo ndio sababu kubwa ya Waislamu kukhitilafiana na kugawanyika makundi makundi. Amesema Imaam Maalik رحمه الله "'Hakuna kitakachotengeneza Ummah huu wa mwisho ila kwa kile kilichotengeneza Ummah wa mwanzo". Na maadam Salafus-Swaalih (watangu wema) hawakufanya bid'ah kama hii, sisi ni lazima tuwe na khofu kubwa ya kuifanya.

SABABU YA TATU:  Ametuamrisha Allaah سبحانه وتعالى tufuate aliyotuletea Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na tujiepushe na aliyotukataza:
    ((وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا))
 ((Na anachokupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni jiepusheni nacho)) [Al-Hashr:7]
 SABABU YA NNE: Kufuata amri ya Kumtii Allaah سبحانه وتعالى na Mtume Wake صلى الله عليه وآله وسلم :
 Anasema Allaah سبحانه وتعالى katika Aayah nyingi kwenye Qur-aan:
 ((وَأَطِيعُوا اللَّهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ))
 ((Na mtiini Allaah na mtiini Mtume )) [At-Twaghaabun:12]
 Na kumtii Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni kumtii Allaah سبحانه وتعالى
 ((مَّنْ يُطِعِ الرَّسُولَ فَقَدْ أَطَاعَ اللّهَ))
 ((Mwenye kumtii Mtume basi ndio amemtii Allaah)) [An-Nisaa:80]
 SABABU YA TANO: Kutokufuata amri ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni kumkhalifu na kupata adhabu kali:
   ((فَلْيَحْذَرِ الَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنْ أَمْرِهِ أَن تُصِيبَهُمْ فِتْنَةٌ أَوْ يُصِيبَهُمْ عَذَابٌ أَلِيم))

((Basi nawatahadhari wanaokhalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu chungu)) [An-Nuur:63]
 SABABU YA SITA:  Kumpinga Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni sababu ya kuingizwa toni:

 ((وَمَن يُشَاقِقِ الرَّسُولَ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُ الْهُدَى وَيَتَّبِعْ غَيْرَ سَبِيلِ الْمُؤْمِنِينَ نُوَلِّهِ مَا تَوَلَّى وَنُصْلِهِ جَهَنَّمَ وَسَاءتْ مَصِيرًا))
 ((Na anayempinga Mtume baada ya kumdhihirikia uongofu, na akafuata njia isiyo kuwa ya Waumini, tutamuelekeza alikoelekea, na tutamuingiza katika Jahannamu. Na hayo ni marejeo maovu)) [An-Nisaa 115]
 SABABU YA SABA: Kukhofu upotofu unaompeleka mtu motoni:
   Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Alikuwa akitanguliza khutba zake kwa kutoa maonyo hayo:
 (( إن خير الكلام كلام الله وخير الهدي هدي محمد صلى الله علي وسلم  وشر الأمور محدثاتها وكل محدثة بدعة وكل بدعة ضلالة وكل ضلالة في النار))  أخرجه مسلم في صحيحه 
 ((Maneno bora  ni kitabu cha Allah (Qur-aan) na Uongofu mbora kabisa ni uongofu wa Muhammad  صلى الله عليه وآله وسلم  na jambo la shari kabisa ni uzushi, na kila jambo jipya (katika dini) ni bid'ah (uzushi)  na kila bid'ah ni motoni)) [Muslim katika Swahiyh yake]
 SABABU YA NANE:  Khofu ya kuwa miongoni mwa kundi litakaloingia motoni:
  Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipoonya katika Hadiyth ifuatayo kuwa makundi yote yanayojiita ni ya Kiislam na hali hayafuati mafunzo kama aliyokuja nayo yeye, yatakuwa motoni isipokuwa kundi moja. Maswahaba walishtuka na wakataka kujua ni kundi gani hilo moja, akawajibu kuwa ni kundi ambalo watu wake watakuwa wanafuata mwendo wake na wa Maswahaba zake.
 ((افترقت اليهود على إحدى وسبعين فرقة، وافترقت النصارى على اثنتين وسبعين فرقة، وستفترق هذه الأمة على ثلاث وسبعين فرقة كلها في النار إلا واحدة،)) فقال الصحابة: من هي يا رسول الله؟ قال: ((من كان على مثل ما أنا عليه وأصحابي)) الترمذي و الحاكم
 ((Waligawanyika Mayahudi katika makundi sabini na moja, na waligawanyika Manaswara katika makundi sabini na mbili, na utagawanyika Umma wangu katika makundi sabini na tatu, yote yataingia motoni ila moja!)) Maswahaba wakasema: 'Ni kundi lipi hilo Ee Mtume wa Allaah?  Akajibu: ((Ni lile ambalo litakuwa katika mwenendo wangu hii leo na Maswahaba zangu)) [Imepokewa na Maimaam At-Tirmidhiy na Al-Haakim]
 SABABU YA TISA: Kuitikia wasiya wa Allaah سبحانه وتعالى  ili kubakia katika njia iliyonyooka:
 Anasema Allaah سبحانه وتعالى :
  ((وَأَنَّ هَذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ وَلاَ تَتَّبِعُواْ السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ذَلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ))
 ((Na kwa hakika hii ndiyo Njia Yangu Iliyonyooka. Basi ifuateni, wala msifuate njia nyingine, zikakutengeni na Njia yake. Haya Amekuusieni ili mpate kumcha Mungu)) [Al-An'aam: 153]
 inaendelea

Sababu za Kutosherehekee Maulidi-Sehemu ya Pili


 Sehemu ya Pili 
 SABABU YA KUMI: Vitendo visivyokuwa vya Sunnah havipokelewi:
  (( من عمل عملاً ليس عليه أمرنا فهو رد)) البخاري
 ((Atakayetenda kitendo kisichokuwa chetu (katika dini yetu) basi kitarudishwa)) [Al-Bukhaariy]
 Hivyo mtu atapoteza muda wake, labda na gharama ya kutekeleza bid'ah hii na kumbe amali hii haina thamani yoyote mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala).
 SABABU YA KUMI NA MOJA: Maulidi  yamezushwa karne ya nne (miaka mia nne) baada ya kufa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  na watu wenye kufru:
 Walioanzisha Maulidi ni viongozi wa Faatwimiyyun huko Misr (hawa walikuwa ni Rawaafidh (Mashia) katika dhehebu la Ismailiyah [Makoja] walianza kusherehekea  Maulidi ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (Radhiya Allahu ‘anhu), na Maulidi ya Hasan na Husayn (Radhiya Allahu ‘anhuma), na Maulidi ya Faatwimah az-Zahraa (Radhiya Allahu ‘anha), na Maulidi ya kiongozi wao aliye hai kwa wakati ule. Sasa kwa nini tuwafuate wao? Na kama alivyotujulisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kwamba watu bora kabisa wa kuwafuata ni wa karne tatu pekee aliposema:
     ((خير الناس قرني ثم الذين يلونهم ثم الذين يلونهم))  متفق عليه 
 ((Watu bora kabisa ni wa karne yangu, kisha wanaowafuatia kisha wanaowafuatia)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
 SABABU YA KUMI NA MBILI: Makafiri wanafurahi Waislamu wanapofanya Bid'ah kwani ni kuacha mafunzo sahihi ya dini na ni kuzifuta Sunnah za Mtume صلى الله عليه وآله وسلم :
 Napoleon Bonaparte alimpa Shaykh Al-Bakriy Riyaal mia  nane za Ufaransa (inasemekana ni mia tatu kwenye sehemu zingine) ili arudishe bid'ah ya Maulidi naye akahudhuria mwenyewe Maulidi. Maana makafiri wanajua kuwa Waislam wanaposhughulishwa na vipumbazo kama hivyo, husahau matakwa yao ya msingi na muhimu.
 SABABU YA KUMI NA TATU: Baadhi ya maneno katika Maulidi yana kufru ya kumpandisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم cheo cha usawa na Allaah سبحانه وتعالى wakati yeye ametuonya tusifanye hivyo:

 ((لا تطروني كما أطرت النصارى المسيح ابن مريم، إنما أنا عبد، فقولوا: عبد الله ورسوله))  متفق عليه

((Msinitukuze Kama Manaswara walivyomtukuza Masiyh mwana wa Maryam, hakika mimi na mja kwa hiyo semeni mja wa Allaah na Mjumbe Wake)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
 SABABU YA KUMI NA NNE:  wanapoinuka kumswalia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم wanaamini kwamba roho yake inahudhuria wakati huo:
 Hii ni fikra ovu kabisa, na pia yeye mwenyewe alikuwa hapendi kuinukiwa alipokuwa hai, vipi mtu anayempenda amfanyie jambo analolichukia wakati amekufa?
 Siku moja Maswahaba walikuwa wamekaa msikitini pamoja na Abubakar رضي الله عنه  ambaye alikuwa akisoma Qur-aan. 'Abdullah ibn Ubbay ibn Saluul, mnafiki mkubwa alikuja akaweka takia na mto wake akaketi. Alikuwa ni mwenye sura nzuri na mwenye lugha ya ufasaha. Alisema: "Ewe Abu Bakar, muulize Mtume صلى الله عليه وآله وسلم atuonyeshe alama ya utume wake kama walivyotuonyesha Watume wengine. Mfano, Muusa عليه السلام  ametuletea Ubao (wa Tauraat), 'Iysa عليه السلام alituletea Injiyl na meza ya chakula kutoka mbinguni, Daawuud عليه السلام alituletea Zabuur, Swaalih عليه السلام alitulietea ngamia wa kike" Abu Bakar رضي الله عنه aliposikia akaanza kulia. Mara akaingia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na Abu Bakar رضي الله عنه akawaambia Maswahaba wengine wainuke kumpa heshima Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na kumpa malalamiko ya mnafiki. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: ((Sikizeni! Msiniinukie mimi bali….
 وَقُومُواْ لِلّهِ قَانِتِينَ
 ((na simameni kwa ajili ya Allaah))  [Al-Baqarah: 238] (dalili kutoka Tafsiyr Ibnu Kathiyr] 
 SABABU YA KUMI NA TANO: Kuchanganyika kwa wanawake na wanaume:
 Jambo ambalo limekatazwa katika dini na katika sherehe hii kumedhihirika sana hasa pande za nchi zetu za Afrika Mashariki. Na uovu huu unafikia hadi kuimba kwa pamoja na kuchezesha vichwa kama kwamba ni dansi fulani. Imefika hadi maulidi kuitwa ‘disco maulidi’
 SABABU YA KUMI NA SITA:  Kuwaigiza Manaswara:  
Manaswara wanasherehekea siku ya kuzaliwa 'Iysa عليه السلام kama wanavyodai. Na Waislamu haitupasi kusherehekea siku ya kuzaliwa  Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  kwani tumefundishwa kuwa tufanye kinyume na wao katika mambo yetu.
Vilevile Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  kasema:
  ((خالفوا المشركين، أحفوا الشوارب، وأوفوا اللحى)) البخاري و مسلم
 ((Kuweni kinyume na Washirikina, punguzeni masharubu na fugeni ndevu)) [Al-Bukhaariy na Muslim]
 Na kufanya hivyo (kusherehekea Maulidi) tutakuwa tunajifananiza nao, na jambo hilo la kuwaiga na kujifananisha na mambo yao limekatazwa kama alivyosema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم :
  ((من تشبه بقوم فهو منهم )) أحمد و أبو داود
 Anayejishabihisha na watu basi naye ni miongoni mwao)) [Ahmad, Abu Daawuud]
 SABABU YA KUMI NA SABA:  Dini imekamilika hakuna tena haja ya kuleta mambo ya dini mapya:
 Kuzusha mambo mapya ya dini ni kama kumtuhumu Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kuwa ametukhini mafunzo ya dini na hakuyakamilisha, bali kuna aliyoyaficha na hakutupa yote!! Na hali aliikamilisha dini kama ilivyompasa. Aayah hii chini iliteremshwa kudhihirisha ukamilifu wa dini ya Mola Mtukufu
   ((الْيَوْمَ أَكْمَلْتُ لَكُمْ دِينَكُمْ وَأَتْمَمْتُ عَلَيْكُمْ نِعْمَتِي وَرَضِيتُ لَكُمُ الإِسْلاَمَ دِينً))
 ((Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na nimekutimizieni Neema Yangu, na Nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini)) [Al-Maaidah:3]
 Sasa vipi watu walete mafundisho ya dini mapya yasiyotokana na mafunzo kutoka kwa Allaah سبحانه وتعالى na Mtume Wake صلى الله عليه وآله وسلم ? Anauliza Allaah سبحانه وتعالى :
 ((أَمْ لَهُمْ شُرَكَاء شَرَعُوا لَهُم مِّنَ الدِّينِ مَا لَمْ يَأْذَن بِهِ اللَّهُ))
 ((Au hao wana miungu ya kishirikina waliowatungia dini asiyoitolea idhini Allaah?)) [Ash-Shuura 21]
 SABABU YA KUMI NA NANE: Kudhihirisha iymaan kwa kupenda yale aliyokuja nayo Mtume صلى الله عليه وآله وسلم pekee:
 عَنْ أَبِي مُحَمَّدٍ عَبْدِ اللَّهِ بِنْ عَمْرُو بِنْ العَاصِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا  قَالَ : قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وآله وسلم: ((لا يُؤْمِنُ أَحَدُكُمْ حَتَّى يَكُونَ هَوَاهُ تَبَعَاً لِمَا جِئْتُ بِهِ )) حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ، رَوَيْنَاهُ فِي كِتَابِ "الْحُجَّةِ  بِإِسْنَادٍ صَحِيحٍ.   
 Kutoka kwa Abu Muhammad Abdullah Ibn 'Amr Bin Al-'Aasw رضي الله عنه ambaye alisema:  Mtume صلى الله عليه وسلم  kasema: ((Hatokuwa kaamini (kikwelikweli) mmoja wenu mpaka mapenzi yake yatakapomili (yatakapotii au kuwafikiana) kwenye yale niliyoyaleta)) (mafundisho) [Hadiyth Hasan iliyotoka katika kitabu “Al-Hujjah” ikiwa na mtiriko mzuri wa mapokezi]
 SABABU YA KUMI NA TISA: Kuacha mambo yenye shaka na kubakia katika yaliyo wazi: 
  عَنْ أَبي مُحمَّدٍ الحسَنِ بْنِ عليّ بْنِ أبي طَالِب، سِبْطِ رَسُولِ اللهِ صلى الله عليه وسلم وَرَيْحَانَتِهِ رضيَ اللهُ عنهُما، قالَ: حَفِظْتُ مِنْ رَسُولِ الله صلى الله عليه وسلم: ((دَعْ ما يَرِيبُكَ إلى مَا لاَ يَرِيُبكَ )) رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ   وَالنَّسَائِيُّ    وَقَالَ التِّرْمِذِيُّ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ. 
 Kutoka kwa Abu Muhammad Al-Hasan Ibn ‘Aliy Ibn Abi Twaalib mjukuu wa Mtume صلى الله عليه وسلم na kipenzi chake رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا  alisema: "Nilihifadhi kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وسلم maneno haya: ((Acha kile kinachokutia shaka ufuate kile kisichokutia shaka)). [Imesimuliwa na At-Tirmidhiy na An-Nasaaiy, At-Tirmidhiy akisema kuwa ni hadiyth Hasan na Swahiyh]
 SABABU YA ISHIRINI: Mwezi huu wa Rabiy'ul Awwal ni mwezi alioaga dunia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم , sasa vipi Muislamu asherehekee?
 Wanachuoni wote wameafikiana kuwa siku hii ya tarehe 12 Rabiy‘ul Awwal ni siku aliyofariki Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Vipi sasa watu watakuwa wanafurahi kwa siku kama hiyo? Anas bin Maalik رضي الله عنه anatuhadithia kuwa: "Hakuna siku ambayo watu wa Madiynah walikuwa na furaha ya hali ya juu kama siku aliyohamia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  katika mji huo. Na hakuna siku ya huzuni kabisa kwa watu wa Madiynah kama siku aliyoaga dunia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ."
 Inaonekana kama sisi tunakwenda kinyume na maadili ya wale watu bora waliokuwa wakimpenda Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hata kuliko nafsi zao wenyewe.
 SABABU YA ISHIRINI NA MOJA:  Sababu za Waislamu wanaoshikilia Bid'ah:  
 1-Kufuata bila ya kupata elimu sahihi.
Ukitaka kujua hoja za Waislamu wanaofuata bid'ah, hutopata kutoka kwao hoja nyingi kutoka katika Qur-aan na Sunnah, bali ni hoja za kutokana na rai zao tu, au watakwambia, 'kwani kuna ubaya gani?'. Na hata wakitoa hoja kutoka katika Qur-aan na Sunnah basi utakuta kwamba wanazifasiri dalili hizo isivyokusudiwa bali wanazishabihisha na matamanio yao kama Anavyosema Allaah سبحانه وتعالى :
 ((هُوَ الَّذِيَ أَنزَلَ عَلَيْكَ الْكِتَابَ مِنْهُ آيَاتٌ مُّحْكَمَاتٌ هُنَّ أُمُّ الْكِتَابِ وَأُخَرُ مُتَشَابِهَاتٌ فَأَمَّا الَّذِينَ في قُلُوبِهِمْ زَيْغٌ فَيَتَّبِعُونَ مَا تَشَابَهَ مِنْهُ ابْتِغَاء الْفِتْنَةِ وَابْتِغَاء تَأْوِيلِه))
 ((Yeye Ndiye Aliyekuteremshia Kitabu (hiki Qur-aan). Ndani yake zimo aayah Muhkam (nyepesi kufahamika) ambazo ndizo msingi (asili) wa Kitabu (hiki). Na ziko nyingine Mutashaabihaat (zinababaisha kama habari ya Akhera, za Peponi na Motoni na mengineyo ambao yamekhusika na Roho). Wale ambao nyoyoni mwao mna upotofu wanafuata zile zinazobabaisha kwa kutaka kuwaharibu watu na kutaka kujua hakika yake vipi)) [Al-'Imraan:7]
 Na ukizingatia utaona kuwa Waislamu wanaofuata Bid'ah sio wenye elimu kubwa ya juu, kwani ukilinganisha na wanaofuata Sunnah utaona kuwa kuna tofauti kubwa sana. Na hivyo ndivyo Allaah سبحانه وتعالى Anavyomjaalia kumpa elimu ya upeo wa juu yule mwenye kufuata haki. Na tujiulize Maulamaa wangapi wacha Mungu wenye elimu madhubuti wanafuata Bid'ah? Si rahisi kuwapata, bali ukiuliza wanaofuata Sunnah na wenye elimu kubwa ambayo athari yake tunaiona leo hii na itaendelea kizazi hadi kizazi InshaAllah, utakuta  ni wengi sana, miongoni mwao ni Maimamu wanne; Imaam Shaafi'iy, Ahmad bin Hanbali, Abu Haniyfah, Maalik, Sufyaan Ath-Thawry. Wasimulizi wa Hadiyth kina Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuud, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Ibn Maajah na kadhalika. Maulamaa maarufu; Ibn Taymiyah, ibnul Qayyim, ibnul Jawzy, ibnul Mubaarak, ibnu Hajar, ibnu Kathiyr, Imaam An-Nawawy, na waliopita katika miaka ya karibuni kama kina: ibn 'Uthaymiyn, ibn Baaz, Shaykh Al-Albaaniy na kadhalika. Hata katika jamii yetu kuna waliokuwa wamejaaliwa kupewa kipaji cha elimu kama kina Shaykh 'Abdullah Swaalih Al-Faarisy na kina Al Amiyn na Muhammad Qaasim Mazrui, Haarith Swaalih na wengineo wengi, bila kuwataja walio hai ambao hawana idadi kwa wingi wao.
 2- Kufuata matamanio ya nafsi
Hufuata matamanio ya nafsi inavyopenda na sio kufuata haki. Wengine kutokana na unasaba wao huwa ni kwao kama utukufu kuwa nao wamo katika unasaba wa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم
Anasema Allaah سبحانه وتعالى :
 ((وَلاَ تَتَّبِعِ الْهَوَى فَيُضِلَّكَ عَن سَبِيلِ اللَّهِ))

((Wala usifuate matamanio yakakupoteza kwenye Njia ya Allaah)) [Swaad:26]

3- Ugumu wa kuacha mila uliotokana na mababa na mababu
Mitume waliopita walikuwa wakiwaita watu wao wawafuate waliyokuja nayo ya haki walipendelea kubakia katika ujinga na mila za mababa zao. Na Waislamu wenye kufuata mambo ya bid'ah nao ni vile vile ukiwauliza kwa nini hamuachi mambo yasiyo katika mafundisho ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم wanajibu hivyo hivyo kuwa 'vipi tuache Maulidi na hali tumekulia nayo?, au tutaachaje kitu ambacho mababa zetu walikuwa wakifanya?? Ina maana wao walikuwa hawajui?"

Anasema Allaah سبحانه وتعالى :
 ((وَإِذَا قِيلَ لَهُمْ تَعَالَوْاْ إِلَى مَا أَنزَلَ اللّهُ وَإِلَى الرَّسُولِ قَالُواْ حَسْبُنَا مَا وَجَدْنَا عَلَيْهِ آبَاءنَا أَوَلَوْ كَانَ آبَاؤُهُمْ لاَ يَعْلَمُونَ شَيْئًا وَلاَ يَهْتَدُون))
 ((Na wanapoambiwa: Njooni kwenye yale Aliyoyateremsha Allaah, na kwa Mtume, husema: Yanatutosha tuliyowakuta nayo baba zetu. Je, hata ikiwa baba zao walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?)) [Al-Maaidah: 104]


Au walikuwa wakisema:
 ((بَلْ قَالُوا إِنَّا وَجَدْنَا آبَاءنَا عَلَى أُمَّةٍ وَإِنَّا عَلَى آثَارِهِم مُّهْتَدُونَ))
((Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunafuata nyayo zao)) [Az-Zukhruf: 22]
 4- Kukhofu kutokuungana na wengi wanaofuata bid'ah
 Wengine ukiwauliza kwa nini unafuata bid'ah ya Maulidi. Jibu ni kuwa anakhofu kuwa yeye peke yake ataonekana kuwa hasomi Maulidi katika kundi lake, na hii ni hatari ya kukhofu watu badala ya kumkhofu Mola Mtukufu na pia ni kwenda na mkumbo kwa kudhani kuwa wengi ndiyo wenye haki! Haya Anatueleza Allaah kuwa:
 ((وَإِن تُطِعْ أَكْثَرَ مَن فِي الأَرْضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ اللّهِ إِن يَتَّبِعُونَ إِلاَّ الظَّنَّ وَإِنْ هُمْ إِلاَّ يَخْرُصُونَ))
 ((Na ukiwatii wengi katika hawa waliomo duniani watakupoteza na Njia ya Allaah. Hawa hawafuati ila dhana tu, na hawakuwa ila ni wenye kusema uwongo tu)) [Al-An'aam: 116]
 5- Wengine wanasema kuwa ni kudhihirisha mapenzi ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم
 Je, mapenzi ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  yadhihirike siku moja tu? Au katika mwezi huu tu? Na si siku zote? Hayo bila shaka ni mapenzi ya uongo. Mapenzi ya kweli ni yale ya kumkumbuka siku zote na kumtii umpendaye. Haya ya Maulidi hayana moja kati ya mawili hayo.

6- Hoja ya kusema ni Bid'atun-hasanah (uzushi mzuri)
Mojawapo yao ni kuwa Maulidi ni Bid'atun-hasanah. Katika dini ya Kiislamu hakuna bid'ah nzuri kwani Mtume صلى الله عليه وآله وسلم   alipotuonya alisema 'Kullu Bid'atin Dhwaalaah' (kila bid'ah ni upotofu). Na ikiwa kauli hii wanaipinga kuwa sio  KILA bid'ah, basi wanasemaje kuhusu kauli ya Allaah سبحانه وتعالى Anaposema:
  ((كُلُّ نَفْسٍ ذَآئِقَةُ الْمَوْتِ))
 ((Kila nafsi itaonja mauti)) [Al-'Imraan:185]
Je, tupinge pia kauli hii kuwa sio KILA nafsi? Na je, ina maana kuwa kuna watu wengine watabakia hawatokufa na hali tunatambua kuwa hakuna atakayebakia ila Mwenyewe Mola Mtukufu?

Tunamuomba Allaah سبحانه وتعالى Atuhidi kwa kutuonyesha yaliyo haki ili tuyafuate na Atuonyeshe yaliyo baatil tujiepushe nayo.
Aamiyn.

 

Website Hit