Mambo Ya Kufanya Siku Ya Ijuma
Assalam alaqum,Tunashukuru mungu kwa kuanza kutumia group hii siku ya ijumaa leo tuanza kwa kuanza kuelezea Mambo Ya Kufanya Siku Ya Ijumaa ni kama ifuatavyo
1 Kukoga (Ghuslu)
ni wajibu ( kukoga kwa kujitia tohara) siku ya Ijumaa ni wajibu kwa kila Muislamu aliyebaleghe.
... 2. Swala ya Ijumaa -
{Enyi mlio amini! Ikiadhiniwa Sala siku ya Ijumaa, nendeni upesi kwenye dhikri ya Mwenyezi Mungu, na wacheni biashara. Hayo ni bora kwenu, lau kama mnajua} (Al-Jumua 62:9 )
3 Kufika mapema msikitini
Kila atakapofika mtu mapema msikitini huwa amepata daraja Fulani na muhimu kabisa
4. Sura ya kusoma siku ya Ijumaa
-Atakayesoma Suratul-Kahf siku ya Ijumaa atakuwa katika mwangaza
5. Kumswalia Mtume:
Kutoka kwa Aws Ibn Aws رضي الله عنه ambaye alisema: Kasema Mtume صلى الله عليه وسلم : Siku bora kabisa kwenu ni siku ya Ijumaa, kwa hiyo zidisheni kuniswalia, kwani Swala (kuniombea kwenu) zenu zinaonyeshwa kwangu (Imehadithiwa na Abu Dawood).
Sourec:Posted by Almudarisu via facebook.com on TANZANIA MUSLIM Group
Comments :
0 comments to “Mambo Ya Kufanya Siku Ya Ijuma”
Post a Comment