Islamic Calender

Powered by Blogger.

Sababu za Kutosherehekee Maulidi-Sehemu ya Kwanza


 sehemu ya kwanza
Sababu 21 Za Kumfanya Muislam Asisherehekee Maulid
 Zifuatazo ni sababu na hoja ambazo Muislam mwenye kupenda kufuata haki na mwenye kutaka apate uongofu ili abakie katika njia iliyonyooka na ajiepushe na mambo ya baatil. Hoja ni za wazi kutoka katika Qur-aan na Sunnah. Hoja za kupinga jambo hili ziko nyingi sana, lakini tulizozikusanya tunatumai kuwa zitamtosheleza Muislamu aikinaishe nafsi yake kuwa Maulidi ni jambo la uzushi katika dini kwa hiyo ni bora kutenda amali zile tulizopata mafundisho yake kutoka kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم, Maswahaba wake na Salafus Swaalih (Watangu wema) .
SABABU YA KWANZA: Kumpenda Mola Mtukufu Aliyetuumba:
Kwanza kabisa ni kwa sababu  ya kumpenda Mola Mtukufu Aliyetuumba Ambaye Anataka kuhakikisha kuwa mapenzi yetu Kwake ni kumfuata Mtume صلى الله عليه وآله وسلم. Naye tokea kuzaliwa kwake hadi kufa kwake hakufanyiwa wala hakusherehekea siku yake ya kuzaliwa. 
 Anasema Allaah سبحانه وتعالى :
 ((قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللّهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللّهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَاللّهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ)) 
 ((Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allaah basi nifuateni mimi, Allaah Atakupendeni na Atakufutieni madhambi yenu. Na Allaah ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu)) [Al-'Imraan: 31] 
 SABABU YA PILI: Kufuata amri yake Mtume صلى الله عليه وآله وسلم    ya kushikamana na Sunnah Zake na Sunnah za Makhalifa wake:
 (( أُوصِيكُمْ بِتَقْوى اللَّه، وَالسَّمْعِ وَالطَّاعَةِ وإِنْ تَأَمَّر عَلَيْكُمْ عَبْدٌ حبشيٌ ، وَأَنَّهُ مَنْ يَعِشْ مِنْكُمْ فَسَيرى اخْتِلافاً كثِيرا . فَعَلَيْكُمْ بسُنَّتي وَسُنَّةِ الْخُلُفَاءِ الرَّاشِدِينَ الْمَهْدِيِّينَ ، عضُّوا عَلَيْهَا بالنَّواجِذِ ، وإِيَّاكُمْ ومُحْدثَاتِ الأُمُورِ فَإِنَّ كُلَّ بِدْعَةٍ ضلالَةٌ ))  رواه أبو داود ، والترمذِي وقال حديث حسن صحيح
((Nakuusieni kumcha Allah, usikivu na twaa hata ikiwa kiongozi wenu (Au atakayekuamrishen) ni Mtumwa  wa Habash. Mtakaoishi miongoni mwenu mtaona ikhtilafu nyingi. Kwa hiyo shikamaneni na Sunnah zangu na Sunnah za Makhalifa waliongoka baada yangu.  Ziumeni kwa magego (zikamateni kwa nguvu wala msiziache). Na tahadharini na mambo ya uzushi kwani kila bid'ah ni upotofu)) [Abu Daawuud, At-Trimidhiy kasema Hadiyth Hasan Swahiyh]   
Kwa hiyo inamtosheleza Muislamu hoja hii pekee ya kuwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم wala Maswahaba zake hawakusherehekea Maulidi, kumfanya naye asisherehekee.
Na hiyo ndio sababu kubwa ya Waislamu kukhitilafiana na kugawanyika makundi makundi. Amesema Imaam Maalik رحمه الله "'Hakuna kitakachotengeneza Ummah huu wa mwisho ila kwa kile kilichotengeneza Ummah wa mwanzo". Na maadam Salafus-Swaalih (watangu wema) hawakufanya bid'ah kama hii, sisi ni lazima tuwe na khofu kubwa ya kuifanya.

SABABU YA TATU:  Ametuamrisha Allaah سبحانه وتعالى tufuate aliyotuletea Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na tujiepushe na aliyotukataza:
    ((وَمَا آتَاكُمُ الرَّسُولُ فَخُذُوهُ وَمَا نَهَاكُمْ عَنْهُ فَانتَهُوا))
 ((Na anachokupeni Mtume chukueni, na anacho kukatazeni jiepusheni nacho)) [Al-Hashr:7]
 SABABU YA NNE: Kufuata amri ya Kumtii Allaah سبحانه وتعالى na Mtume Wake صلى الله عليه وآله وسلم :
 Anasema Allaah سبحانه وتعالى katika Aayah nyingi kwenye Qur-aan:
 ((وَأَطِيعُوا اللَّهَ وَأَطِيعُوا الرَّسُولَ))
 ((Na mtiini Allaah na mtiini Mtume )) [At-Twaghaabun:12]
 Na kumtii Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni kumtii Allaah سبحانه وتعالى
 ((مَّنْ يُطِعِ الرَّسُولَ فَقَدْ أَطَاعَ اللّهَ))
 ((Mwenye kumtii Mtume basi ndio amemtii Allaah)) [An-Nisaa:80]
 SABABU YA TANO: Kutokufuata amri ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni kumkhalifu na kupata adhabu kali:
   ((فَلْيَحْذَرِ الَّذِينَ يُخَالِفُونَ عَنْ أَمْرِهِ أَن تُصِيبَهُمْ فِتْنَةٌ أَوْ يُصِيبَهُمْ عَذَابٌ أَلِيم))

((Basi nawatahadhari wanaokhalifu amri yake, usije ukawapata msiba au ikawapata adhabu chungu)) [An-Nuur:63]
 SABABU YA SITA:  Kumpinga Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ni sababu ya kuingizwa toni:

 ((وَمَن يُشَاقِقِ الرَّسُولَ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُ الْهُدَى وَيَتَّبِعْ غَيْرَ سَبِيلِ الْمُؤْمِنِينَ نُوَلِّهِ مَا تَوَلَّى وَنُصْلِهِ جَهَنَّمَ وَسَاءتْ مَصِيرًا))
 ((Na anayempinga Mtume baada ya kumdhihirikia uongofu, na akafuata njia isiyo kuwa ya Waumini, tutamuelekeza alikoelekea, na tutamuingiza katika Jahannamu. Na hayo ni marejeo maovu)) [An-Nisaa 115]
 SABABU YA SABA: Kukhofu upotofu unaompeleka mtu motoni:
   Mtume صلى الله عليه وآله وسلم Alikuwa akitanguliza khutba zake kwa kutoa maonyo hayo:
 (( إن خير الكلام كلام الله وخير الهدي هدي محمد صلى الله علي وسلم  وشر الأمور محدثاتها وكل محدثة بدعة وكل بدعة ضلالة وكل ضلالة في النار))  أخرجه مسلم في صحيحه 
 ((Maneno bora  ni kitabu cha Allah (Qur-aan) na Uongofu mbora kabisa ni uongofu wa Muhammad  صلى الله عليه وآله وسلم  na jambo la shari kabisa ni uzushi, na kila jambo jipya (katika dini) ni bid'ah (uzushi)  na kila bid'ah ni motoni)) [Muslim katika Swahiyh yake]
 SABABU YA NANE:  Khofu ya kuwa miongoni mwa kundi litakaloingia motoni:
  Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alipoonya katika Hadiyth ifuatayo kuwa makundi yote yanayojiita ni ya Kiislam na hali hayafuati mafunzo kama aliyokuja nayo yeye, yatakuwa motoni isipokuwa kundi moja. Maswahaba walishtuka na wakataka kujua ni kundi gani hilo moja, akawajibu kuwa ni kundi ambalo watu wake watakuwa wanafuata mwendo wake na wa Maswahaba zake.
 ((افترقت اليهود على إحدى وسبعين فرقة، وافترقت النصارى على اثنتين وسبعين فرقة، وستفترق هذه الأمة على ثلاث وسبعين فرقة كلها في النار إلا واحدة،)) فقال الصحابة: من هي يا رسول الله؟ قال: ((من كان على مثل ما أنا عليه وأصحابي)) الترمذي و الحاكم
 ((Waligawanyika Mayahudi katika makundi sabini na moja, na waligawanyika Manaswara katika makundi sabini na mbili, na utagawanyika Umma wangu katika makundi sabini na tatu, yote yataingia motoni ila moja!)) Maswahaba wakasema: 'Ni kundi lipi hilo Ee Mtume wa Allaah?  Akajibu: ((Ni lile ambalo litakuwa katika mwenendo wangu hii leo na Maswahaba zangu)) [Imepokewa na Maimaam At-Tirmidhiy na Al-Haakim]
 SABABU YA TISA: Kuitikia wasiya wa Allaah سبحانه وتعالى  ili kubakia katika njia iliyonyooka:
 Anasema Allaah سبحانه وتعالى :
  ((وَأَنَّ هَذَا صِرَاطِي مُسْتَقِيمًا فَاتَّبِعُوهُ وَلاَ تَتَّبِعُواْ السُّبُلَ فَتَفَرَّقَ بِكُمْ عَن سَبِيلِهِ ذَلِكُمْ وَصَّاكُم بِهِ لَعَلَّكُمْ تَتَّقُونَ))
 ((Na kwa hakika hii ndiyo Njia Yangu Iliyonyooka. Basi ifuateni, wala msifuate njia nyingine, zikakutengeni na Njia yake. Haya Amekuusieni ili mpate kumcha Mungu)) [Al-An'aam: 153]
 inaendelea

Comments :

0 comments to “Sababu za Kutosherehekee Maulidi-Sehemu ya Kwanza”

Post a Comment

 

Website Hit